News
Hotuba ya Wizara ya Miundombinu2009/10 - Mh. Dr. Shukuru Kawambwa (MB.)
A: UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwa leo ndani ya Bunge lako tukufu na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako tukufu likubali upokea, kujadili na kupitisha Mpango wa Maendeleo na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Miundombinu...
A: UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwa leo ndani ya Bunge lako tukufu na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako tukufu likubali upokea, kujadili na kupitisha Mpango wa Maendeleo na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Miundombinu kwa mwaka wa fedha 2009/10. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kuchukua fursa hii kutoa pole kwako binafsi na Bunge lako tukufu kutokana na vifo vya Waheshimiwa Wabunge wafuatao: Mheshimiwa Zakayo Chacha Wangwe, Mheshimiwa Richard Nyaulawa na Mheshimiwa Faustine Kabuzi Rwilomba. Vifo vya Wabunge hawa vimeleta majonzi makubwa kwa Bunge, wananchi wa majimbo ya Tarime, Mbeya Vijijini na Busanda ,familia za marehemu na Taifa kwa ujumla. Tutawakumbuka marehemu Wabunge hawa kwa michango yao mikubwa katika maendeleo ya nchi yetu. Mungu azilaze roho za marehemu Wabunge hawa mahali pema peponi - Amin.

